COASCO YAZIDI KUIMARISHA UTENDAJI KUPITIA VIKAO VYA WATUMISHI VYA KILA MWEZI
COASCO YAZIDI KUIMARISHA UTENDAJI KUPITIA VIKAO VYA WATUMISHI VYA KILA MWEZI
Watumishi wa Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) wamefanya kikao cha kila mwezi kwa lengo la kusikiliza maoni, mapendekezo na changamoto mbalimbali ili kuimarisha utendaji wa Shirika.
Kikao hicho kimefanyika Machi 25, 2026 katika Ofisi ya Makao Makuu ya COASCO jijini Dodoma, na kuongozwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, CPA Prisilla Mushi, aliyemwakilisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, CPA Jeremiah Mugeta.
