Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO)

COASO Logo
Majukumu yetu

a) Kutoa huduma za Ukaguzi wa hesabu kwa Vyama vya Ushirika, vikundi vya ushirika, Makampuni binafsi au ya umma,pamoja na taasisi nyingine;

b) Kutoa huduma ya usimamizi kwa vikundi vya ushirika na Vyama vya Ushirika;

c) Kuandaa Sera, kanuni, miongozo, taratibu za kiutendaji, masuala ya uwekezaji na mpango wa biashara

d) Kutoa huduma za Ushauri wa kitaalamu katika masuala ya kodi, uhasibu, fedha, uwekezaji, utawala, usimamizi wa vihatarishi na Utafiti kwa Vyama vya Ushirika

e) Kusimamia makampuni mengine ya ukaguzi yatakayotoa huduma za Ukaguzi kwa Vyama vya Ushirika

f)Kufanya Ukaguzi maalum na uchunguzi (Special Audits and Investigation)

g) Kufanya jambo lolote lenye kurahisisha utendaji wa majukumu ya Shirika.

h) Kuendesha mafunzo ya kazi/vitendo kwa vyama vya ushirika kuhusu utunzaji wa vitabu vya hesabu na utayarishaji wa taarifa za fedha kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Kuripoti Taarifa za Fedha (IFRSs), Uhasibu, Usimamizi wa fedha, uongozi na utawala bora