KAMATI YA BODI YA COASCO YAKUTANA KUJADILI MASUALA YA AJIRA, MAENDELEO YA UTUMISHI NA UTAWALA
10 Jun, 2026
KAMATI YA BODI YA COASCO YAKUTANA KUJADILI MASUALA YA AJIRA, MAENDELEO YA UTUMISHI NA UTAWALA
Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limeendesha kikao cha Kamati ya Bodi ya Ajira, Maendeleo ya Utumishi na Utawala kwa lengo la kupitia na kujadili masuala mbalimbali ya rasilimali watu, ajira, maendeleo ya watumishi, utawala pamoja na mpango wa mawasiliano na matumizi ya vyombo vya habari.
Kikao hicho kimefanyika leo, Juni 9, 2026 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Shirika jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa COASCO kinachotarajiwa kufanyika Juni 11, 2026.
