KAMATI ZA BODI YA COASCO ZAPITIA NA KUJADILI TAARIFA ZA UKAGUZI, USIMAMIZI WA VIHATARISHI, UCHUMI NA MIPANGO
10 Jun, 2026
KAMATI ZA BODI YA COASCO ZAPITIA NA KUJADILI TAARIFA ZA UKAGUZI, USIMAMIZI WA VIHATARISHI, UCHUMI NA MIPANGO
Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limeendesha vikao vya Kamati ya Bodi ya Ukaguzi na Usimamizi wa Vihatarishi pamoja na Kamati ya Mipango na Uchumi kwa lengo la kupitia na kujadili ripoti ya Mkaguzi wa Ndani wa Shirika, taarifa ya usimamizi wa vihatarishi na taarifa ya utendaji wa Shirika.
Vikao hivyo vimefanyika leo, Juni 8, 2026 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Shirika jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa COASCO kinachotarajiwa kufanyika Juni 11, 2026.
