MWONGOZO WA PAMOJA WA UKAGUZI WA NJE WA VYAMA VYA USHIRIKA KATI YA COASCO NA TCDC
21 Dec, 2024
Pakua
Mwongozo huu umeandaliwa kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Vyama vya ushirika Na. 6 ya mwaka 2013, Kanuni zake za mwaka 2015, na sheria ya Ukaguzi na Usimamizi wa vyama vya Ushirika sura ya 185. Lengo kuu la Mwongozo huu ni kuhakikisha ukaguzi wa hesabu katika Vyama vya Ushirika unatekelezwa ipasavyo, kwa kuzingatia Sheria na Miongozo mbalimbali. Hivyo, COASCO na TCDC wanatarajia kwamba Mwongozo huu utakuwa nyenzo muhimu katika kurahisisha huduma ya ukaguzi katika Vyama vya Ushirika.